NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo amezitaka halmashauri kuwawezesha vijana na kinamama kwa vitendo kwa kuyapa makundi hayo baadhi ya kazi zilizo chini ya halmashauri ambazo wanao uwezo wa kuzifanya ili wajiongezee kipato.

Jafo ameyasema hayo leo katika hafla ya kukabidhi hundi ya Sh. milioni 70 iliyotolewa na Manispaa ya Dodoma kwa vikundi vya ujasiliamali vya vijana na kinamama ndani ya manispaa hiyo.

Ameeleza kwamba haipendezi kwa halmashauri yeyote kuwanyima fursa ya kazi vikundi vya vijana na kinamama ambapo kazi hizo zinaweza kufanywa na makundi hayo.

Jafo ametolea mfano kikundi cha vijana cha DOYODO ambacho kina kiwanda cha kisasa cha kufyatua Matofali lakini wanahangaika soko  la kuuzia matofali wakati kuna ujenzi mkubwa wa madarasa na vyoo unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Wawakilishi wa vikundi vya vijana na kinamama wa Manispaa ya Dodoma wakipokea hundi ya Sh.Milioni 70 kwa ajili ya shughuli za ujasiriamali.
 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Selemani Jafo akizungumza na wajasiriamali wa Manispaa ya Dodoma katika hafla ya kukabidhi hundi ya Sh.Milioni 70 kwa ajili ya vikundi vya Kinamama na Vijana.
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi akitoa taarifa ya mikopo ya vijana na kinamama kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi Selemani Jafo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...