Rais Dkt John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo mafupi mara baada kufungua mradi wa ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Tabora. Rais Dkt Magufuli ameagiza Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano kujenga jengo la abiria 500 badala ya jengo lililopo la abiria 50.Pia ameagiza urefu wa uwanja uongezwe hadi kufikia kilometa 2.5 badala ya kilometa 1.9 zilizopangwa ili ndege kubwa na ndogo ziweze kuutumia uwanja huo.
Rais Dkt John Pombe Magufuli ameweka jiwe la Msingi la mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda miji ya Tabora, Nzega na Igunga. Mradi huo utagharimu Shilingi Bilioni 600 na unatekelezwa kwa fedha za mkopo nafuu kutoka India. Una uwezo wa kuzalisha lita Milioni 80 kwa ajili ya Mji wa Tabora.
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo mafupi ya mradi huo wa ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Tabora,kutoka kwa Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano,Prof Makame Mbarawa mapema leo mkoani humo

Rais Dkt John Pombe Magufuli mapema leo amefungua mradi wa ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Tabora,Wakati wa uzinduzi wa mradi huo,Rais Dkt Magufuli ameagiza Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano kujenga jengo la abiria 500 badala ya jengo lililopo la abiria 50.Pia ameagiza urefu wa uwanja uongezwe hadi kufikia kilometa 2.5 badala ya kilometa 1.9 zilizopangwa ili ndege kubwa na ndogo ziweze kuutumia uwanja huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...