Na Hamza Temba - Dodoma
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe.
Dk. Hamisi Kigwangalla ameipongeza Serikali ya Finland kwa ushirikiano na
misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikiitoa kuunga mkono juhudi za Serikali
katika uhifadhi wa maliasili na uendelezaji wa misitu nchini.
Dk. Kigwangalla ametoa pongezi
hizo leo Januari 16, 2018 kwa Balozi wa nchi hiyo hapa nchini, Mhe. Peka Huka
ambaye amemtembelea ofisini kwake mjini Dodoma kwa ajili ya kujitambulisha na
kujadili mambo mbalimbali ya kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo katika
uhifadhi na maendeleo ya misitu nchini.
“Napenda kutoa pongezi zangu za
dhati kwa Serikali ya Finland, mmekuwa washirika
wetu wakubwa wa maendeleo kwa muda mrefu ambao mmetusaidia mambo mbalimbali
ikiwemo kuendeleza misitu nchini, kuendeleza Chuo cha Mafunzo ya Misitu
Olmotonyi na hata mapitio ya Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 1998, ni
matumaini yetu kuwa mtaendelea kudumisha ushirikiano huu”, alisema Dk.
Kigwangalla.
Alimueleza balozi huyo kuwa
Tanzania inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika uhifadhi wa misitu nchini
ikiwemo uhaba wa rasilimali fedha na teknolojia kwa ajili ya kuwezesha uhifadhi
endelevu. Alisema changamoto nyingine ni uvunaji haramu wa mazao ya misitu ambayo
husababisha eneo la hekta 372,000 za misitu kupotea kila mwaka.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Peka Huka ofisini kwake mjini Dodoma leo alipotembelewa na balozi huyo kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo katika uhifadhi na uendelezaji wa misitu nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi
Kigwangalla (kulia) akimkaribisha Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Peka Huka
ofisini kwake mjini Dodoma leo alipotembelewa na balozi huyo kwa ajili ya
kujitambulisha na kujadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano baina ya
nchi hizo katika uhifadhi na uendelezaji wa misitu nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na Balozi wa Finland hapa nchini, Mhe. Peka Huka ofisini kwake mjini Dodoma leo alipotembelewa na balozi huyo kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili mambo mbalimbali ya kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo katika uhifadhi na uendelezaji wa misitu nchini.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...