Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), Mheshimiwa Lolensia Bukwimba akizungumza katika kikao cha Kamati hiyo ambapo imekutana na uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kujadili na kuchambua Taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji na utendaji wa Taasisi hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo ambapo imekutana na uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kujadili na kuchambua Taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji na utendaji wa Taasisi hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC)wakati Kamati ilipokutana na Taasisi hiyo kwa ajili ya kujadili na kuchambua Taarifa ya Msajili wa Hazina kuhusu uwekezaji na utendaji wa Taasisi hiyo.kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini ya JKCI, Profesa William Mahalu. Kikao hicho kimefanyika leo katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira wakiwa katika kikao cha Kamati hiyo ambapo leo walikuwa wakijadili ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Shirikisho la wenye Viwanda Nchini (CTI).Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mheshimiwa Sadiq Murad akikisitiza jambo katika kikao cha Kamati hiyo ambapo leo walikuwa wakijadili ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Shirikisho la wenye Viwanda Nchini (CTI).Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Bunge Mjini Dodoma. PICHA NA OFISI YA BUNGE
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...