Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

NAIBU Waziri wa Madini, Dotto Biteko amelitaka Shirika la Taifa la Madini (Stamico) kujitathini kuhusu utendaji wao wa kazi kwa Taifa kutokana na kuwa deni kubwa kuliko uzalishaji wa shirika hilo.

Biteko ametoa kauli hiyo alipotembelea Shirika la Taifa la Madini (Stamico) leo, Dar es Salaam,ambapo amesema Stamico imekuwa na madeni yanayofanya kudidimiza shirika kutokana na miradi wanayoiendesha ya uchimbaji kushindwa kuzalisha faida.

Amesema baada ya watu kujua changamoto sasa ndio wameona sehemu kujengea hoja katika taarifa mbalimbali.Biteko amesema Stamico ilitakiwa kuwa sehemu ya kujifunzia kwa wachimbaji wadogo lakini wachimbaji wadogo hawawezi kufika Stamico kwa sababu hakuna cha kujifunza.

Stamico inadeni zaidi ya Sh.bilioni moja pamoja na deni la Stamigold la Sh.bilioni 54 na Serikali inatakiwa kulipa deni hilo na kuacha kununua madawati katika shule.Biteko amesema kuwa kunahitajika kuwepo ubunifu kwa Stamico kwa kujiona wana kazi ya ziada ya kusaidia Taifa kupiga hatua.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Stamico, Alex Rutagwelela amesema kuwa maagizo watayafanyia kazi katika uendeshaji wa shirika hilo.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akikagua mtambo wa uchongaji mashimo kwa ajili ya utafiti wakati alipotembelea Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza wakati wa kikao cha pamoja na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akisitiza wakati wa kikao cha pamoja na Uongozi pamoja na watumishi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Dotto Mashaka Biteko akiwa katika picha ya  pamoja na Uongozi wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Mtaa wa Upanga Jijini Dar es salaam, Leo 16 Januari 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...